BRIGEDIA JENERALI STEPHEN MNKANDE
Administration Title MKUU WA CHUO

WASIFU

Brigedia Jenerali Stephen Mnkande ni Mkuu wa 18 kukiongoza Chuo cha Ukamanda na Unadhimu – Duluti. Aliteuliwa kushika madaraka hayo Julai 13, 2023 na kukabidhiwa Ofisi rasmi na mtangulizi wake Brigedia Jenerali Sylvester Ghuliku Julai 31, 2023.

Brigedia Jenerali Mnkande alijiunga na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania Machi 12, 1993 baada ya kuhitimu Mafunzo ya Awali ya Kijeshi. Alihudhuria Kozi ya Afisa Mwanafunzi katika Chuo cha Maafisa Wanafunzi Monduli (TMA) kuanzia mwaka 1993 na kupata Kamisheni Juni 25, 1994 na kutunukiwa cheo cha Luteni Usu.

Baada ya Kamisheni alihudhuria Kozi mbalimbali ndani na nje ya nchi ifuatavyo:-

  • Kozi ya Ulinzi wa Taifa (NDC), mwaka 2016/17 nchini Tanzania;
  • Kozi ya Juu ya Ukamanda na Unadhimu (Advanced CSC), mwaka 2011 nchini Wingereza;
  • Kozi ya Ukamanda na Unadhimu (CSC), mwaka 2008 nchini Uganda;
  • Kozi ndogo ya Ukamanda na Unadhimu (JC & SC), mwaka 2003 nchini Zimbabwe;
  • Kozi ya Uongozi wa Kombania, mwaka 2001 nchini Tanzania;
  • Kozi ya Ukufunzi, mwaka 1998 nchini Tanzania;
  • Kozi ya Ungozi wa Patuni, mwaka 1997 nchini Tanzania; na
  • Kozi ya Awali ya Uhandisi wa Medani, mwaka 1996 nchini Tanzania.

Aidha, kabla ya kuteuliwa kuwa Kaimu Mkuu wa Chuo ameshika nyadhifa mbalimbali ndani ya JWTZ na nje ya Jeshi ifuatavyo:-

  • Mnadhimu Elekezi Mwandamizi Jeshi la Nchi Kavu – NDC – Tanzania, 2022 – 2023;
  • Brigedi Kamanda FIB – MUNUSCO, 2021 – 2022;
  • Kaimu Mkuu wa Tawi la Mipango na Maendeleo Jeshini, 2020 – 2021;
  • Mkurugenzi wa “Doctrine” Jeshini, 2019 – 2020;
  • Kaimu Mkuu wa Chuo cha Maafisa Wanafunzi (TMA), 2018- 2019;
  • Mkufunzi Mkuu Chuo cha Maafisa Wanafunzi (TMA), 2017 – 2018;
  • Msaidizi namba mbili wa Mkuu wa Majeshi (MA – 2 to CDF), 2015 – 2016;
  • Mnadhimu Elekezi wa Mpango wa Kubadilishana (DS on Exchange Programme) CSC nchini Zimbabwe, 2012 – 2014;
  • Mnadhimu Elekezi CSC – Tanzania, 2009 – 2012;
  • Kozi Kamanda wa Maafisa Wanafunzi (Officer Cadets) – TMA, 2005 – 2007;
  • Mkufunzi wa kozi za Kamanda wa Patuni na Kombania – TMA, 1999 – 2007;
  • Kamanda wa Patuni – TMA, 1999 – 2004;
  • Kozi Kamanda wa Kozi za Uhandisi wa Medani – 121 FER, 1997 – 1998;
  • Mkufunzi wa Kozi za Uhandisi wa Medani– 121 FER, 1996 – 1998; na
  • Kamanda wa Patuni ya Uhandisi wa Medani (Troop Commander) – 121 FER, 1996.

Vile vile ametunukiwa Medali ifuatavyo:-

  • Medali ya Utumishi Uliotukuka. Tanzania;
  • Medali ya Utumishi Mrefu, Tanzania;
  • Medali ya Miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika;
  • Medali ya Miaka 50 ya Muungano wa Tanzania;
  • Medali ya Miaka 50 ya JWTZ;
  • Medali ya Comoro na Anjuan;
  • Medali ya Miaka 40 ya JWTZ;
  • Medali ya Miaka 30 ya JWTZ; na
  • UN Medals (UNAMSIL and MUNUSCO).

Brigedia Jenerali Mnkande anapenda kufanya Mazoezi ya kukimbia (jogging), Kusoma, Kuangalia Makala za Programu mbali mbali, na kusikiliza Mijadala ya Kimkakati.